Kampeni ya kundi la watu imefanikiwa
kukusanya kiasi cha dola 40,000 ili kumsaidia mshindi wa medali ya
fedha katika mbio za marathoni Feyisa Lilesa wa Ethiopia ili kupata
hifadhi.
Lilesa alimaliza mbio hizo za
Olimpiki huku akionyesha ishara jamii ya Oromo ya Ethiopia,
wanayotumia kupingana na serikali na uamuzi wa kutaka kutwaa eneo la
jamii hiyo.
Mwanariadha huyo amesema anaweza
kuuwawa iwapo atarejea nyumbani Ethiopia, hata hivyo serikali imesema
itampokea kama shujaa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni