.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 18 Agosti 2016

NEYMAR AIONGOZA BRAZIL KUICHAKAZA HONDURA MAGOLI 6-0

Neymar amefunga katika sekunde ya 14, likiwa ni goli la mapema mno kufungwa katika historia ya michuano ya Olimpiki, wakati Brazil ikiichakaza bila huruma Hondura kwa magoli 6-0 na kutinga fainali.

Wenyeji Brazil watakutana na Ujerumani ikiwa na kumbukumbu ya kufungwa magoli 7-1 katika kombe la dunia 2014, hii ni baada ya kuitoa Nigeria kwa magoli 2-0 yaliyofungwa na Lukas Klostermann na Nils Petersen.

Katika ushindi huo uliofufua matumaini kwa Brazil kutwaa ubingwa, Neymar na Gabriel Jesus walifunga magoli mara mbili.
                      Neymar akifunga goli la kwanza ndani ya sekunde 14 tu ya mchezo 
                                      Neymar akiwa angani akiuangalia mpira ukiingia golini
  Neymar akigugumia maumivu ya kifua baada ya kuangukia kifua wakati wa kufunga goli hilo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni