




Wizara ya Maji na Umwagiliaji leo imesaini Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano kati yake na Shirika lisilo la Serikali, Tanzania Water Partnership (TWP) kwa ajili ya utekelezaji wa Utunzaji na Usimamizi wa Rasilimali za Maji nchini.
Makubaliano hayo yalisainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Inj. Mbogo Futakamba na Mtendaji Mkuu wa Tanzania Water Partnership, Dkt. Victor Kongo na kuhudhuriwa na wataalamu kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji na wajumbe kutoka Tanzania Water Partnership.
Lengo kuu la ushirikiano huo likiwa ni kutunza na kusimamia rasilimali za maji nchini kwa ajili ya maendeleo endelevu ya upatikanaji wa maji nchini na kuinua kiwango cha huduma ya majisafi na salama kwa wananchi wote Tanzania.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni