Mamia ya wakazi wa Jiji la Nairobi
watakosa maji kwa siku mbili baada ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji
Taka ya Jiji la Nairobi kupanga kufunga kwa muda mtambo wa kusafishia maji wa
Ngethu kwa matengenezo.
Mamlaka hiyo ya maji ya Jiji na
Nairobi, hii leo imetangaza kukosekana kwa huduma ya maji katika siku
za Alhamisi na Ijumaa wiki hii.
Mtambo wa kusafisha maji wa Ngethu
hutoa huduma ya maji kwa asilimi 85 ya wakazi wa Jiji la Nairobi.
Mtambo huo unafungwa kwa muda ili kubadilishwa valvu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni