Kikundi cha kujilinda kimesema kuwa
wapiganaji wa Boko Haram wameshambulia kijiji kimoja kaskazini
mashariki mwa Nigeria na kumkata kichwa chifu wa kijiji hicho na
mtoto wake wa kiume.
Kikundi hicho cha Abbas Gavi cha wananchi wa Nigeria, kimesema wapiganaji hao wa Boko Haram walivamia kijiji hicho
cha Tallari jumatatu kabla ya mapambazuko.
Wamesema wapiganaji hao walimkata
shingo chifu wa kijiji hicho Ba' Lawan pamoja na mtoto wake wa kiume
na kuichoma moto nyumba yake pamoja na nyingine kijijini hapo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni