Jaji mstaafu nchini Australia
ameomba kubadilishana nafasi na mkimbizi ili jaji huyo aweze kuishi
maisha yake aliyobakia katika kambi zinazoshikilia wakimbizi nchini
humo.
Jaji mstaafu Jim Macken, 88, amesema
amemuandikia Waziri wa Uhamiaji wa Australia, Peter Dutton, ili aweze
kubadilishana na mkimbizi mmoja ili yeye achukue nafasi yake ya
ukimbizi.
Jaji mstaafu Macken amesema anaelewa
kuwa ombi lake hilo si la kawaida, lakini anaomba atekelezewa kwa
moyo safi kabisa.
Hali ilivyo katika moja ya kambi inayoshikilia wakimbizi Australia
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni