Mkurugenzi Mtendaji wa The Guardian Limited, Richard Mgamba ( katikati )
akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu
kampuni hiyo kudhamini mashindano ya Miss Tanzania 2016. Kulia ni
Mkurugenzi wa Lino Agency waandaaji wa shindano hilo, Hashim Lundega na
kushoto ni mjumbe wa kamati hiyo Mary Eammanuel
Mkurugenzi
wa Radio One Stereo, Deogratius Rweyunga akizungumza wakati Kampuni ya
The Guardian Limeted ilipotangaza kudhamnini mashindano ya Miss Tanzania
2016. Kulia kwake ni mjumbe wa kamati hiyo Mary Eammanuel akifuatiwa na Mkurugenzi
Mtendaji wa The Guardian Limited, Richard Mgamba. Wengine ni mkuu wa Itifaki Albert Makoye ( mwenye tai ) na mjumbe Shah.
Kampuni
ya magazeti ya The Guardian Limited imejitosa kuyadhamini mashindano ya
Miss Tanzania 2016 ambayo yanaandaliwa na kampuni ya Lino International
Agency Limited.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi
Mtendaji wa The Guardian Limited, Richard Mgamba amesema kampuni hiyo
imeamua kudhamini mashindano hayo kutokana na ubora wake, na pia kupitia
mashindano hayo baadhi ya washiriki huonyesha vipaji vyao.
"
Sisi kama chombo cha habari moja ya malengo yetu ni kutoa habari,
burudani, kudumisha utamaduni na kusimamia yale yote mazuri yanayoleta
amani na mshikamano katika nchi yetu, alisema Mgamba ambaye kampuni yake
ni wachapishaji wa magazeti ya The Guardian, The Guardian On Sunday,
Nipashe, Nipashe Jumapili, Taifa Letu na Sema Usikike.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni
ya Lino International Agency Limited, Hshim Lundega aliishukuru The
Guardian kwa kujitokeza kudhamini mashindano hayo na kusema mwaka huu
wameyaboresha zaidi na watanzania watarajie shindano lenye msisimko wa
kipekee.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni