KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR AFUNGUA SKULI YA MSINGI YA ABDALLAH SHARIA
Mkurugenzi Idara ya Elimu Maandalizi na Msingi Bi. Safia Ali Rijali akimkaribisha Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mfunzo ya Amali Zanzibar Bi. Khadija Bakari Juma (hayupo pichani) aliemuakilisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali katika sherehe ya ufunguzi wa Skuli ya Abdallah Sharia iliyopo Tomondo Mjini Zanzibar.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mfunzo ya Amali Zanzibar Bi. Khadija Bakari Juma akizungumza na wananchi na wanafunzi waliofika katika sherehe ya ufunguzi wa Skuli ya Abdallah Sharia iliyopo Tomondo Mjini Zanzibar.
Mbunge mstaafu wa Dimani Abdallah Sharia Amer akizunguma na wananchi wa Tomondo katika sherehe ya ufunguzi wa Skuli ya Abdallah Sharia iliyopo Tomondo Mjini Zanzibar.
Baadhi ya walimu na walikwa waliofika katika sherehe ya ufunguzi wa Skuli ya Abdallah Sharia wakimsikiliza Mgeni rasmin (hayupo pichani) Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mfunzo ya Amali Bi. Khadija Bakari Juma.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mfunzo ya Amali Zanzibar Bi. Khadija Bakari Juma akifungua pazia kwa niaba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali kuashiria ufunguzi wa Skuli ya Abdallah Sharia iliyopo Tomondo Mjini Zanzibar
Muonekano wa Skuli ya Msingi ya Abdallah Sharia iliyopo Tomondo. Picha na Makame Mshenga / Maelezo Zanzibar.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni