Kifaa kinachotiliwa shaka
kilichokutwa karibu na reli Mjini New Jersey kimelipuka wakati
wataalam wa mabomu wakijaribu kukizima kwa kutumia roboti.
Kifaa hicho ni miongoni mwa vitano
vilivyopatikana kwenye begi la mgongoni lililotupwa kwenye takataka
karibu na Elizabeth, kwa mujibu wa meya wa Jiji hilo.
Kubainika kwa vifaa hivyo vya
milipuko kunafuatia shambulizi la mwishoni mwa wiki la mabomu Jijini
New York na New Jersey na tukio la shambulizi la kisu huko Minnesota.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni