.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 19 Septemba 2016

KIFAA KINACHOTILIWA SHAKA CHALIPUKA NEWS JERSY NCHINI MAREKANI

Kifaa kinachotiliwa shaka kilichokutwa karibu na reli Mjini New Jersey kimelipuka wakati wataalam wa mabomu wakijaribu kukizima kwa kutumia roboti.

Kifaa hicho ni miongoni mwa vitano vilivyopatikana kwenye begi la mgongoni lililotupwa kwenye takataka karibu na Elizabeth, kwa mujibu wa meya wa Jiji hilo.

Kubainika kwa vifaa hivyo vya milipuko kunafuatia shambulizi la mwishoni mwa wiki la mabomu Jijini New York na New Jersey na tukio la shambulizi la kisu huko Minnesota. 
 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni