.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 10 Septemba 2016

KOREA KASKAZINI YADAI KUGUNDUA DAWA INAYOTIBU UKIMWI NA EBOLA

Mamlaka za nchini Korea Kaskazini zimesema kuwa wanasayansi wake wamefanikiwa kutengeneza dawa ambayo inauwezo wa kuizuia na kuponya magonjwa kama Ukimwi, Ebola, Mers, Sars na Saratani.

Shirika la Habari la Korea (KNCNA) limesema wanasayansi hao wametengeneza dawa hiyo iitwayo Kumdang-2 kutokana na mmea wa ginseng uliopandwa kwa mbolea iliyochanganywa na madini mbalimbali yakiwemo ya dhahabu na platinum.

Magonjwa kama ya Sars, Ebola na Mers ambayo yanauhusiano na mfumo wa kinga yanaweza kuponywa kwa urahisi na sindano ya dawa ya Kumdang-2 ambayo inasemekana inaongeza kinga imara mno mwilini.
                                      Boksi lenye vichupa vya dawa ya sindano ya Kumdang-2
            Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un akifurahia ugunduzi huo na wanasayansi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni