.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 17 Septemba 2016

LIVERPOOL YAIZAMISHA CHELSEA NYUMBANI KWAO KATIKA DIMBA LA STAMFORD BRIDGE

Timu ya Liverpool imeendeleza kufanya vizuri katika Ligi Kuu ya Uingereza na kuiharibia rekodi Chelsea ya kutofungwa katika msimu huu, kwa kuipa kipigo cha magoli 2-1 katika dimba la Stamford Bridge.

Katika mchezo huo Liverpool ambayo mchezo uliopita iliwafunga mabingwa watetezi Leicester City kwa magoli 4-1, ilianza kwa kasi kipindi cha kwanza na kuandika goli kupitia Dejan Lovren na kisha Jordan Henderson akaongeza la pili.

Beki wa Chelsea, aliyenunuliwa kwa paundi milioni 32, David Luiz, akiichezea Chelsea kwa mara ya kwanza akichukua nafasi ya John Terry ambaye ni majeruhi alisaidia Chelsea kupata goli moja kupitia kwa Diego Costa.
                            Jordan Henderson akifunga goli la shuti la umbali wa yadi 30
                      Diego Costa akipongezwa baada ya kuifungia Chelsea goli pekee 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni