Timu ya Liverpool imeendeleza
kufanya vizuri katika Ligi Kuu ya Uingereza na kuiharibia rekodi
Chelsea ya kutofungwa katika msimu huu, kwa kuipa kipigo cha magoli
2-1 katika dimba la Stamford Bridge.
Katika mchezo huo Liverpool ambayo
mchezo uliopita iliwafunga mabingwa watetezi Leicester City kwa
magoli 4-1, ilianza kwa kasi kipindi cha kwanza na kuandika goli
kupitia Dejan Lovren na kisha Jordan
Henderson akaongeza la pili.
Beki wa Chelsea, aliyenunuliwa kwa
paundi milioni 32, David Luiz, akiichezea Chelsea kwa mara ya kwanza
akichukua nafasi ya John Terry ambaye ni majeruhi alisaidia Chelsea
kupata goli moja kupitia kwa Diego Costa.
Jordan Henderson akifunga goli la shuti la umbali wa yadi 30
Diego Costa akipongezwa baada ya kuifungia Chelsea goli pekee
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni