Mechi mbili za raundi ya sita za Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Majimaji, na African Lyon na Kagera Sugar sasa zitachezwa kwenye Uwanja wa Taifa badala ya Uwanja wa Uhuru.
Mabadiliko hayo yametokana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kusitisha kwa muda kuutumia Uwanja wa Uhuru katika kipindi hiki ambacho limeanza kufanyia marekebisho sehemu ya uwanja huo ambayo ni ya nyasi bandia (artificial turf).
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://tff.or.tz/news/607-mechi-za-simba-lyon-kuchezwa-taifa
BOCCO MCHEZAJI BORA WA AGOSTI
Mshambuliaji John Bocco wa Azam FC amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom wa mwezi Agosti kwa msimu wa 2016/2017.
Bocco ambaye pia ni nahodha wa Azam FC aliwashinda wachezaji Mzamiru Yasin wa Simba na Said Kipao wa JKT Ruvu. Katika mechi mbili ilizocheza katika mwezi huo, Bocco aliifungia timu yake mabao matatu likiwemo la kusawazisha dhidi ya African Lyon.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://tff.or.tz/news/606-bocco-mchezaji-bora-wa-agosti
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni