.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 21 Septemba 2016

MECHI ZA SIMBA, LYON KUCHEZWA TAIFA

Mechi mbili za raundi ya sita za Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Majimaji, na African Lyon na Kagera Sugar sasa zitachezwa kwenye Uwanja wa Taifa badala ya Uwanja wa Uhuru.

Mabadiliko hayo yametokana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kusitisha kwa muda kuutumia Uwanja wa Uhuru katika kipindi hiki ambacho limeanza kufanyia marekebisho sehemu ya uwanja huo ambayo ni ya nyasi bandia (artificial turf).
 

 Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini 

http://tff.or.tz/news/607-mechi-za-simba-lyon-kuchezwa-taifa

BOCCO MCHEZAJI BORA WA AGOSTI

Mshambuliaji John Bocco wa Azam FC amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom wa mwezi Agosti kwa msimu wa 2016/2017.

Bocco ambaye pia ni nahodha wa Azam FC aliwashinda wachezaji Mzamiru Yasin wa Simba na Said Kipao wa JKT Ruvu. Katika mechi mbili ilizocheza katika mwezi huo, Bocco aliifungia timu yake mabao matatu likiwemo la kusawazisha dhidi ya African Lyon.

                                   Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
 

http://tff.or.tz/news/606-bocco-mchezaji-bora-wa-agosti

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni