Maelfu wamehamishwa kutoka kwenye
miji nchini Hispania ambayo pia imefurika watalii kufuatia moto
mkubwa wa nyika eneo la Costa Blanca.
Picha zilizopigwa zinaonyesha moto
mkubwa karibu na eneo la Xabia, kusini mwa Valencia huku kukiwa na
hofu kuwa moto huo umewashwa kwa makusudi jana.
Watalii wa nje na ndani pamoja na
wakazi wa miji iliyokumbwa na moto huo wamehamishiwa kwenye majengo
ya shule na hoteli, huku nyumba 20 zikiwa zimeteketea kwa moto.
Moto wa nyika ukiteketeza majengo katika Costa Blanca
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni