.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 9 Septemba 2016

MSAFARA WA MAKAMU WA RAIS WAPATA AJALI ENEO LA NANGURUWE MKOANI MTWARA

Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( Jwtz ) wakiangalia ndani ya gari aina ya Toyota Land Cruise baada ya kupata ajali.

Watu wanne wamejeruhiwa na kukimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Mtwara, baada ya moja kati ya magari yaliyokuwa katika msafara wa Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hasssan Kupata ajali.

Ajali hiyo imetokea katika eneo la Nanguruwe takribani kilomita 45 kutoka Mtwara mjini.

Ajali hiyo imetokea wakati Makamu wa Rais alipokuwa njiani kuelekea wilayani Tandahimba kutembelea kiwanda cha kubangua korosho cha Amama ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu mkoani mtwara.
  Majeruhi wakipata huduma ya kwanza kabla ya kukimbizwa hospitali kwa matibabu zaidi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni