.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 11 Septemba 2016

TIMU YA LIVERPOOL YAIPATIA KIPIGO KIZITO LEICESTER CITY

Liverpool imewashinda kirahisi mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Uingereza Leicester katika mchezo wao wa kwanza wakichezea katika dimba la nyumbani katika msimu huu.

Wekundu hao walionekana hawakamatiki baada ya Roberto Firmino kuunganisha pande la James Milner na kuandika goli la kwanza, kicha Daniel Sturridge kutoa pasi ya kisigino iliyofungwa na Sadio Mane.

Hata hivyo Leicester ilifufua matumaini pale pasi safi ya Lucas kunaswa na mshambuliaji wao machachari Jamie Vardy na kutikisa nyavu. Hata hivyo Adam Lallana akaongeza lingine na kisha Firmino kufunga la nne kufuatia pasi ya Mane.
                          Roberto Firmino  akitoka nduki kushangilia goli lake alilofunga
           Jamie Vardy akiokota mpira wavuni baada ya kufunga goli pekee la Leicester City

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni