FIFA limeleta mfumo huo unaoitwa GPX yaani Global Players Exchange ambao malengo yake ni kurahisisha kufanya usajili kwa mchezaji mmoja kwenda timu nyingine lakini kabla ya kufanya hivyo utasaidia kupata taarifa kamili za mchezaji huyo na shabaha kuu ni kurahisisha mawasiliano ya TMS Managers nchi nzima, klabu na mashirikisho mbalimbali duniani.
GPX ni kama mtandao wa kijamii unaoweza kulinganishwa na ‘WhatsApp’ unaofanya kuwa na mawasiliano ya karibu na FIFA imeagiza kuwa ni lazima mameneja wa TMS wa kila klabu na mashirikisho ya ya mpira wa miguu kujiunga na mtandao huo ambao si tu kwamba utafanya kazi katika nchi husika, bali pia unaunganisha ulimwengu wote.
Kwa mameneja wa usajili wa timu za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (SFDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) watakaokuwa tayari basi hawana budi kuwasiliana na Meneja Usajili wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ili kupata maelezo ya kina ya namna ya kujiunga na mtandao wa GPX.
MALINZI AMPONGEZA RAIS MPYA WA EFA
Rais
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma
salamu za pongeza kwa Hani Abou-Reida kwa kuchaguliwa kwake kuwa Rais
Mpya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Misri (EFA) katika uchaguzu mkuu
uliofanyika juzi Jumanne Agosti 30, 2016 jijini Cairo.
Katika
salamu zake, Rais Malinzi ameelezea kuwa kuchaguliwa kwa Hani
Abou-Reida katika wadhifa huo ni kilelelezo cha familia ya mpira wa
miguu ya Misri kuona umuhimu wake katika kutumikia shirikishi hilo
sambamba na kuwa mwakilishi FIFA.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini:
MAKOCHA KILIMANJARO QUEENS WATAJWA
Shirikisho
la Mpira Miguu Tanzania (TFF) limemteua Sebastian Nkoma kuwa Kocha Mkuu
wa timu ya soka taifa ya wanawake wa Tanzania Bara maarufu kwa jina la
Kilimanjaro Queens ambayo kwa mara ya kwanza inakwenda kushiriki
mashindano ya kuwania Kombe la Afrika Mashariki na Kati yatakayofanyika
kwa siku tisa kuanzia Septemba 11, 2016 jijini Jinja, Uganda.
Uteuzi
huo wa Nkoma unakwenda sambamba na wasaidizi wake, ambao ni Hilda
Masanche na Edna Lema wakati Meneja wa timu hiyo, Furaha Francis. Mtunza
vifaa ni Esther Chabruma maarufu kwa jina la Lunyamila.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni