Wafanyabiashara wa tikiti maji wakitumia tukio la kupatwa kwa jua katika mji wa Rujewa wilayani Mbarali kuuza matunda hayo kwa wananchi waliofika katika eneo maalum lililotengwa kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa Jua.
Wafanyabiashara wa Mchele wao pia hawakubaki nyuma wakatumia fursa hiyo kuuza Mchele kwa wananchi waliofika kushuhdia tukio hilo.
Mkuu
wa Mkoa wa Mbeya,Amosi Makala,(katikati) ,Mkuu wa Mkoa wa Songwe ,Chiku
Galawa na Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa(TANAPA)
Pascal Shelutete wakitizama tukio la kupatwa kwa jua ka kutumia miwani
maalumu za kutizamia.
Hatua
ya mwanzo ya tukio la kupatwa kwa jua ,baada ya mwezi kuanza kupita
mbele ya Jua na kuanza kuzuia mwanga usifike katika uso wa Dunia.
Benki ya NMB pia walitoa huduma ya kufungua Akaunti kwa wananchi waliofika katika eneo hilo kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ,Amosi Makala akizungumza juu ya fursa za kiuchumi zilizojitokeza kutokana na tukio la kupatwa kwa jua katika mji wa Rujewa wilayani Mbarali.
Mkuu wa Mkoa wa Songe Luteni Mstaafu ,Chiku Galawa akizungumza na wananchi waliofika katika eneo hilo kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua.
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa,TANAPA ,Pascal Sheluetete akizungumza na wanahabari ambapo shirika hilo limetangaza kufungua lango la Ikoga kwa ajili ya kuingia Hifadhi ya Taifa ya Ruaha kwa upande wa Bonde la Ihefu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni