.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 1 Septemba 2016

YONDAN ABAKI, STARS IKIIFUATA NIGERIA

Sentahafu wa Young Africans, Kelvin Yondani si miongoni mwa wachezaji 18 walioondoka leo Septemba mosi, 2016 kwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2017).

Taarifa ambazo Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imezipata ni kwamba Yondani ana matatizo ya kifamilia ambako hajayaweka sawa hadi timu hiyo inaondoka kwenda Nigeria na Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa hajajaza nafasi hiyo.

Mkwasa amekerwa na kitendo hicho, lakini TFF itasubiri ripoti ya kocha huyo mara baada ya kurejea kutoka Nigeria.

Timu hiyo imeondoka na wachezaji 18 huku ikitarajiwa kuungana na na Nahodha wa timu hiyo, Mbwana Samatta nchini Nigeria. Samatta - Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayechezea timu ya Genk ya Ubelgiji anatokea jijini Brussels ambako makocha wake wamemwomba Mkwasa na Daktari wa Taifa Stars, Richard Yomba kumwangalia namna ya kumtumia kwa sababu ya uchovu wa mechi nzito zilizoipa matokeo mazuri ya kutinga hatua ya makundi ya Uropa Ndogo.

Taifa Stars inakwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo huo dhidi ya timu ya taifa ya nchi hiyo, Super Eagles utakaofanyika Septemba 3, 2016.

Licha ya mchezo huo kuwa sehemu ya mchuano wa kuwania nafasi ya kucheza fainali hizo za AFCON 2017 huko Gabon, lakini utakuwa ni wa kukamilisha ratiba baada ya Misri kufuzu kwa fainali hizo kutoka kundi G ambalo mbali ya Nigeria na Tanzania, pia ilikuwako Chad ambayo iliyojitoa katikati ya mashindano.

Wachezaji waliosafiri ni:

Makipa- 


Said Kipao – JKT Ruvu 
Aishi Manula – Azam FC

Mabeki

Vicent Andrew - Young Africans 

Mwinyi Haji - Young Africans 
Mohamed Hussein – Simba SC 
Shomari Kapombe - Azam FC 
David Mwantika - Azam FC

Viungo

Himid Mao - Azam FC 

Shiza Kichuya – Simba SC 
Ibrahim Jeba – Mtibwa Sugar 
Jonas Mkude – Simba SC 
Muzamiru Yassin – Simba SC 
Juma Mahadhi - Young Africans 
Farid Mussa Tenerif ya Hispania

Washambuliaji

Jamal Mnyate – Simba 

Simon Msuva - Young Africans 
Ibrahim Ajib – Simba SC 
John Bocco - Azam FC 
Mbwana Samatta –KRC Genk ya Ubelgiji

Viongozi waliosafiri na timu hiyo ni:

Ahmed Mgoyi - Mkuu wa msafara 

Charles Boniface Mkwasa- Kocha Mkuu 
Hemedi Morocco – Kocha Msaidizi 
Hussein Swedi – Mtunza Vifaa

Richard Yomba – Daktari wa timu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni