.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 1 Novemba 2016

EL-MAAMRY KUKUTANA NA SIMBA, YOUNG AFRICANS NOVEMBA 3

Msuluhishi wa kisheria wa sakata la madai ya Simba dhidi ya Young Africans hali kadhalika Mchezaji Hassan Hamisi Ramadhani maarufu kama Hassan Kessy, Wakili Msomi, Mzee Said El-Maamry anatarajiwa kukutana na pande zinazopingana Alhamisi Novemba 3, mwaka huu ili kufikia mwafaka wa mwadai hayo.

Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji iliagiza pande za Simba na Young Africans kumaliza suala hilo mapema mwezi uliopita, lakini kwa sababu zilizo nje ya TFF na Kamati yake walishindwa kufanya hivyo kupewa barua ya wito kuitwa kikaoni Oktoba 29, mwaka huu.

Hata hivyo, msuluhishi huyo alishindwa kuendelea na kikao hicho baada ya taarifa kutoka Young Africans kusema kwamba mmoja wa Wawakilishi wake, Wakili Msomi Alex Mgongolwa kuwa safarini Iringa alikokwenda kwa sababu ya matatizo ya kifamilia. Ilielezwa kuwa Mgongolwa ambaye ni Mwanasheria wa Young Africans, alifiwa hivyo kuomba kupangiwa siku nyingine.

Kutokana na hali hiyo, E-Maamry amepanga sasa kukutana nna viongozi na/ au Wawakilishi wa pande zote mbili Alhamisi saa 11.00 jioni kwenye ofisi za TFF ili kuketi chini ya kuangalia namna ya kumaliza madai ya Simba iliyowasilisha mashauri mawili ambako moja ni dhidi ya Young Africans ilihali jingine ni dhidi ya mchezaji Hassan Kessy.

Mzee El-Maamry amesema: “Ili kutenda haki, lazima tutoe nafasi kwa pande zote kusikiliszwa. Ni vema Mwanasheria wa Young Africans akasubiriwa.”

Kamati ya TFF inasuburi makubaliano hayo, na ikitokea imeshindikana, suala hilo litarudi kwenye Kamati hiyo kwa ajili ya uamuzi wa mwisho kwa mujibu wa taratibu, kanuni na sheria zinazoongoza mpira wa miguu.


RAUNDI YA 14 LIGI KUU YA VODACOM
 

Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) inatarajiwa kuendelea kesho kwa viwanja sita ambako kwa mara ya kwanza timu zote za Dar es Salaam zitakuwa mikoani kupambana kutafuta nafasi bora katika ligi hiyo iliyoanza Agosti 20, 2016 kabla kufifikia ukomo wa mzunguko wa 15, Novemba 12, mwaka huu.

Vinara ligi hiyo kwenye msimamo msimu wa 2016/17, Simba SC watakuwa wageni wa Stand United kwenye Uwanja wa CCM Kambarage wakati mabingwa watetezi wa taji hilo Young Africans itakaribishwa na Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
 

http://tff.or.tz/news/654-raundi-ya-14-ligi-kuu-ya-vodacom

TAIFA STARS KUJIPIMA NA ZIMBABWE


Baada ya kukosa mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Ethiopia, timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imepata mwaliko wa kucheza na Zimbabwe katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa unaotarajiwa kufanyika jijini Harare, Novemba 13, mwaka huu.

Kama ilivyotokea kwa Ethiopia kuomba nafasi hiyo kwa Tanzania, pia Zimbabwe imefanya hivyo na mara moja Tanzania imethibitisha kucheza mchezo huo wa kirafiki wa kimataifa wenye kutoa tathmini ubora ili kuingia kwenye viwango vya ubora vya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
 

http://tff.or.tz/news/653-taifa-stars-kujipima-na-zimbabwe

SERENGETI BOYS YAANZA KAMBI SAFARI YA KOREA KUSINI
 

Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 – Serengeti Boys, imeanza rasmi kambi ya wiki moja kabla ya kwenda Korea Kusini ambako itashiriki michuano maalumu ya kimataifa iliyoandaliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Korea Kusini.

Timu hiyo itapiga kambi kwa wiki moja kwenye Hosteli za TFF zilizoko Uwanja wa Kumbukumbiu ya Karume, Ilala jijini Dar es Salaam. Tayari vijana wameripoti kwenye hosteli hizo tangu jana Oktoba 31, 2016.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini 


http://tff.or.tz/news/652-serengeti-boys-yaanza-kambi-safari-ya-korea-kusini

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni