.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 24 Novemba 2016

FC ROSTOV YAIPATIA KIPIGO CHA KUSHTUKIZA BAYERN MUNICH

Timu ya Bayern Munich itamaliza katika nafasi ya pili katika Ligi ya Mabingwa Ulaya kundi D baada ya kupata kipigo cha kushtukiza cha magoli 3-2 kutoka kwa FC Rostov ya Urusi.

Timu hiyo ya Ligi Kuu ya Urusi ilipata ushindi wake huo wa kwanza kati Ligi ya Mabingwa Ulaya katika mchezo huo uliochezwa kwenye hali ya hewa ya nyuzi joto -4.

Kwa matokeo hayo FC Rostov inakuwa timu ya kwanza ya Urusi kuwahi kuifunga timu kubwa ya ligi ya Bundesliga katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
  Cristian Noboa akishangilia goli lake la mpira wa adhabu lililofanya matokeo kuwa 3-2
Katika mchezo mwingine Atletico Madrid imeibuka na ushindi wa magoli mawili kwa bila dhidi ya PSV Eindhoven, magoli yaliyofungwa na Gameiro na Griezmann.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni