.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 7 Novemba 2016

MANCHESTER UNITED YAZINDUKA LIGI KUU YA UINGEREZA NA KUPATA USHINDI

Timu ya Manchester United imemaliza ukame wa kutokushinda michezo minne ya Ligi Kuu ya Uingereza kwa kuifunga Swansea City kwa magoli 3-1.

Manchester United iliutawala mchezo huo tangu mwanzoni na kufanikiwa kufunga magoli 3-0 hadi mapumziko, Paul Pogba akifunga goli la shuti kali huku Zlatan Ibrahimovic akitupia mawili.

Mike van der Hoorn aliifungia goli Swansea kipindi cha pili huku wageni Manchester United wakionekana kutotishiwa na safu ya Swansea, katika mchezo huo ambao kocha Jose Mourinho aliushuhudia akiwa jukwaani baada ya kufungiwa.
                          Zlatan Ibrahimovic akiachia shuti lililoza goli lake la kwanza hapo jana 
                         Zlatan Ibrahimovic akishangilia goli lake kwa kuruka teke la kung fu 
       Kipa Fabianski akiruka bila ya mafanikio kuzuia mpira wa shuti kali la Paul Pogba

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni