Zimekuweko taarifa mbalimbali kwenye vyombo vya habari na mitandao kuwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limeandaa shindano maalum mwezi Desemba.
Mwezi Desemba hakuna shindano lolote jipya litakalaondaliwa na TFF zaidi ya mashindano yake ya kawaida ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL) na Azam Sports Federation Cup (ASFC).
Michuano mingine inayosimamiwa na TFF ni Ligi Kuu ya Taifa ya Wanawake (TWPL), Ligi Kuu ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 (TFFU20L), Ligi Daraja la Kwanza (FDL), Ligi Daraja la Pili (SDL) na Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL).
Ikumbukwe tu kwamba kwa sasa, timu za VPL ziko likizo na ni wakati wa Klabu kufanya mchakato wa usajili wa Dirisha Dogo. Duru la pili lenye mizunguko 15 inatarajiwa kuanza Desemba 17, 2016 kama ilivyopangwa hapo awali.
MWANSASU AITA 12 KUIVAA UGANDA DESEMBA 9
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya mpira wa miguu unaochezwa ufukweni (Beach Soccer), John Mwansasu ameita kikosi cha wachezaji 12 kati ya 13 wanaotarajiwa kuivaa Uganda katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa Desemba 9, 2016 utakaofanyika Dar es Salaam.
Mwansasu ambaye hivi karibuni kikosi chake kilicheza na Ivory Coast katika michezo miwili ya kuwania nafasi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa soka la ufukweni bila mafanikio ni makipa ambao ni Rajab Galla na Khalifa Mgaya.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://www.tff.or.tz/news/694-mwansasu-aita-12-kuivaa-uganda-desemba-9
TAARIFA YA KAMATI YA NIDHAMU YA TFF
Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limefuta adhabu iliyotolewa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi (Kamati ya Saa 72) kwa viongozi na wachezaji wa Kimondo.
Kamati ya Saa 72, ilifanya tathmini ya mchezo huo Na. 23 kati ya Kurugenzi na Kimondo ambako iliamua kuwafungia viongozi wa Kimondo, Eric Ambakisye, Selestine Mashenzi, na Mussa Minga kwa miezi sita na kupigwa faini ya Sh. 500,000 kila mmoja.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://www.tff.or.tz/news/693-taarifa-ya-kamati-ya-nidhamu-ya-tff-2
TAARIFA YA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA HADHI ZA WACHEZAJI
Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji ilikutana jana Jumapili Novemba 27, 2016 kwenye Ukumbi wa Mikutano ya Bodi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia mashauri manane.
Shauri la 1. Klabu ya Simba dhidi ya Young Africans na mchezaji Hassan Hamis Ramadhani Kessy
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://www.tff.or.tz/news/691-taarifa-ya-kamati-ya-katiba-sheria-na-hadhi-za-wachezaji
MALINZI AMPONGEZA MTAKA, AAHIDI USHIRIKIANO RT
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amempongeza Anthony Mtaka kwa kuchaguliwa tena kuwa Rais wa Chama cha Riadha Tanzania (RT) - katika uongozi utakaodumu miaka minne ijayo.
Kadhalika, Rais Malinzi amewapongeza wajumbe waliochaguliwa kadhalika Baraza la Michezo la Taifa (BMT), chini ya Mwenyekiti wake, Dioniz Malinzi kwa kufanikisha uchaguzi mkuu wa RT, uliofanyika mjini Morogoro Jumapili.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://www.tff.or.tz/news/690-malinzi-ampongeza-mtaka-aahidi-ushirikiano-rt

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni