Rais wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu Ulimwenguni (FIFA), Bw. Gianni Infantino ametuma salamu za rambirambi kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Bw. Jamal Emil Malinzi kutokana na kifo cha ghafla cha Mchezaji.
Mchezaji aliyekutwa na mauti ni Ismail Mrisho Khalfan. Alifariki dunia baada ya kuanguka uwanjani Desemba 4, 2016 kwenye Uwanja wa Kaitaba, Kagera wakati timu yake ya Mbao ikicheza na Mwadui katika mechi ya ligi ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 20.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://www.tff.or.tz/news/721-infantino-atuma-salamu-za-rambirambi-2
MAJINA YA TIMU ZA TAIFA U23
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetoa nafasi kwa wafamilia wa soka kupendekeza majina ya timu za Taifa za vijana wenye umri wa chini ya miaka 23 za wanawake na wanaume.
Timu hizo za Taifa ya Wanawake U23 na Timu ya Taifa ya Wanaume U23, zitaingia kwenye program ya kuandaliwa kuwania nafasi ya kucheza fainali za michuano ya Olimpiki zitazayofanyika jijini Tokyo, Japan; mwaka 2020.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://www.tff.or.tz/news/720-majina-ya-timu-za-taifa-u23

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni