.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 3 Desemba 2016

RIPHAT HAMISI MCHEZAJI BORA WA VPL MWEZI NOVEMBA, 2016

Mchezaji Riphat Hamisi wa timu ya Ndanda FC amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom wa mwezi Novemba kwa msimu wa 2016/2017.

Riphat ambaye ni mshambulaji aliwashinda wachezaji Shaban Idd wa Azam FC na Mbaraka Abeid wa Kagera Sugar.

Katika mechi mbili ambazo timu ya Ndanda FC ilicheza kwa mwezi huo, Riphat aliisaidia timu yake kupata ushindi katika michezo yote na kukusanya jumla ya pointi 6 zilizoifanya kushika nafasi ya kumi katika msimamo wa Ligi hiyo ambayo iko mapumzikoni kupisha dirisha dogo la usajili.

Pia aliifungia timu yake mabao mawili katika michezo miwili ambayo timu yake ilicheza kwa mwezi huo.

Mwezi huo ulikuwa na raundi mbili zilizochezwa. Kwa kushinda tuzo hiyo, Riphat atazawadiwa kitita cha sh. milioni moja kutoka kwa wadhamini wa Ligi hiyo, kampuni ya Vodacom Tanzania.

DURU LA KWANZA LIGI YA TFFU20

Ligi ya vijana kwa timu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom inaendelea katika vituo viwili vya Kagera na Dar Es Salaam ambapo duru la kwanza linatarajiwa kumalizika Desemba 05, 2016.


Katika kituo cha Dar es Salaam, Simba ya Dar es Salaam inatarajiwa kucheza kesho Jumapili Novemba 4, 2016 na JKT Ruvu ya Pwani katika mchezo utakaoanza saa 8.00 mchana wakati saa 10.30 kutakuwa na mchezo kati ya Tanzania Prisons ya Mbeya na Ndanda FC ya Mtwara.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

http://www.tff.or.tz/news/699-duru-la-kwanza-ligi-ya-tffu20

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni