.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 28 Januari 2017

TOTTENHAM YAPONEA CHUPUCHUPU KUTOLEWA KWENYE KOMBE LA FA

Son Heung-min amefunga goli katika dakika za mwisho na kuisaidia Tottenham kuibuka na ushindi, ikitokea kuwa nyuma goli moja dhidi ya timu ya daraja la pili ya Wycombe katika mchezo wa kombe la FA,

Mchezaji Paul Hayes, ambaye awali mpira uligonga mwamba aliishtua timu ya Ligi Kuu ya Uingereza kwa goli la shuti la mguu wa kushoto na kuifanya Wycombe iongoze kwa goli moja.

Kapteni huyo wa Wycombe alifunga goli la pili kwa mwaju wa penati, hata hivyo goli la Son na la penati lililofungwa na Vincent Janssen na matokeo kuwa 2-2.

Garry Thomson aliyetokea benchi alifunga kwa kicha mpira wa krosi ya Myles Weston na kuifanya Waycombe iongoze tena lakini Dele Alli alisawazisha na Son kufunga goli la nne la ushindi.

                   Garry Thomson akifunga goli baada ya kutokea benchi katika mchezo huo 
                  Son Heung-min akifunga goli la ushindi la Tottenham katika dakika ya 90+7

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni