.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 23 Februari 2017

RAIS MALINZI AELEZA MIKAKATI, NAPE AIPONGEZA TFF

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi ameelezea mikakati mbalimbali ya maendeleo ya soka nchini akisema hiyo ndiyo sababu ya Kamati ya Utendaji kubuni na kuunda Mfuko wa Maendeleo ya soka.

Katika Risala yake aliyoitoa jana mbele ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mheshimiwa Nape Nnauye katika uzinduzi wa mfuko huo, Rais Malinzi alisema wamefanya hivyo kwa lengo la kutimiza ndoto za Tanzania kushiriki michuano mbalimbali ya soka.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

http://tff.or.tz/news/802-rais-malinzi-aeleza-mikakati-nape-aipongeza-tff

UAMUZI WA KIKAO CHA SAA 72

Kikao cha Bodi ya Kusimamia na Kuendesha Ligi, kiliketi mwanzoni mwa wiki hii na kufanya tathmini ya mambo mbalimbali yaliyotokea kwenye michezo mbalimbali ya mpira wa miguu kwa michuano yote – Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili.

Haya haya ndiyo yaliyojiti katika kila mchezo.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

http://tff.or.tz/news/801-uamuzi-wa-kikao-cha-saa-72

AZAM SPORTS FEDERATION CUP KUENDELEA KESHO

Baada ya Simba kutangulia robo fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) yaani Azam Sports Federation Cup kwa kuifunga African Lyon kwa bao 1-0, mechi nyingine za kuwania nafasi hiyo zitaanza kuchezwa kesho Ijumaa Februari 24, mwaka huu.

Simba iliilaza African Lyon katika mchezo wa hatua ya 16 bora uliofanyika Februari 16, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

http://tff.or.tz/news/800-azam-sports-federation-cup-kuendelea-kesho

LIGI KUU YA WANAWAKE SASA KUANZA FEBRUARI 26

Ligi Kuu ya Wanawake ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) hatua ya 6 Bora itaanza rasmi Februari 26, 2017 kwenye kituo kimoja cha Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala, Dar es Salaam.

Timu sita zilizofanikiwa kufika hatua ya Sita Bora ni JKT Queens ya Dar es Salaam, Mlandizi Queens ya Pwani na Fair Play ya Tanga kutoka Kundi “A” wakati kutoka Kundi “B” zimo Marsh Acedemy ya Mwanza, Sisterz ya Kigoma na Panama ya Iringa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni