.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 13 Machi 2017

HARRY KANE ANAWEZA KUWA NJE YA UWANJA KATIKA MSIMU WOTE

Harry Kane anaweza kuwa nje ya uwanja katika msimu huu wote baada ya kuumia enka katika mchezo wa FA ambao Tottenham walishinda kwa magoli 6-0 dhidi ya Millwall.

Mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Uingereza alitoka katika dimba la White Hart Lane akiwa na magongo, na kufungwa mguu wake kwa buti la kitabibu.

Kocha wa Spurs Mauricio Pochettino amelinganisha jeraha alilopata Kane, sawa na alilopata mwezi Septemba mwaka jana na kumuweka nje ya uwanja kwa wiki saba.
                Mguu wa Harry Kane ulioumia ukiwa kati kati ya miguu ya beki wa Millwall
    Kiwiko cha mguu wa Harry Kane kikipinda na kuumia baada ya kukaliwa na beki wa Millwall

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni