.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 1 Machi 2017

JUVENTUS YAIFUNGA NAPOLI KATIKA KOMBE LA KOPA ITALIA

Paulo Dybala amefunga kwa mikwaju miwili ya penati wakati Juventus ikiifunga Napoli kwa magoli 3-1 katika mchezo wao wa nusu fainali ya kwanza wa kombe la Coppa Italia.

Alikuwa Jose Callejon aliyewapatia wageni goli la kuongoza baada ya kufanya shambulizi nzuri, lakini Muargentina Dybala alisawazisha kwa mkwaju wa penati.

Gonzalo Higuain aliwafungia wenyeji goli la pili kabla ya baadaye Dybala kuongeza goli la tatu baada ya kipa Pepe Reina kumuangusha Juan Cuadrado. 
                                                      Paulo Dybala akifunga goli kwa mkwaju wa penati
                                          Gonzalo Higuain akifunga goli la pili katika mchezo huo 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni