.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 2 Machi 2017

MOUSSA DEMBELE AZIDI KUTAKATA CELTIC IKIJIKITA ZAIDI KILELENI

Celtic imefikisha rekodi ya kucheza mechi 22 za Ligi Kuu ya Scotland bila ya kufungwa na kuongoza kwa tofauti ya pointi 27, ikihitaji pointi saba tu kutwaa ubingwa kwa mara sita mfululizo.

Katika mchezo huo wa jana dhidi ya Inverness, Celtic iliutawala mpira lakini ilibidi ingojee hadi katika dakika ya 43 ya mchezo, kabla ya Scott Sinclair kufunga goli zuri la shuti la kuzungusha.

Goli lao la pili lilipatikana katika sekunde ya 12 ya kipindi cha pili baada ya Moussa Dembele akitumbukiza kimiani kwa mpira.

Stuart Armstrong alifunga goli kwa mpira wa adhabu na kisha Dembele akafunga goli lake la pili na la nne katika mchezo huo na kufanya matokeo kuwa 4-0.
                                 Moussa Dembele akifunga goli kwa kuubetua kidogo mpira juu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni