.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 31 Machi 2017

MZUNGUKO WA 25 VPL WIKIENDI HII, AFRICAN LYON v STAND UTD SAA 8.00 MCHANA

Baada ya kusimama kwa muda wa takribani wiki tatu kupisha michuano mbalimbali ya kimataifa kwa ngazi ya timu ya taifa na klabu, kadhalika michuano ya Kombe la Azam Sports Federation Cup, Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) inarejea tena kesho Jumamosi kwa michezo miwili.

Michezo ya kesho Jumamosi Aprili mosi, mwaka huu itakuwa kati ya Mabingwa watetezi wa VPL, Young Africans na Azam - mechi itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati mchezo mwingine utakuwa ni kati ya Mbeya City na Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya. Mechi zote za Jumamosi, zitafanyika saa 10.00 jioni.
 

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
 

http://tff.or.tz/news/840-mzunguko-wa-25-ligi-kuu-ya-vodacom 

GHANA KUTUA, SERENGETI BOYS KUIVAA TENA BURUNDI
 

Timu ya taifa ya vijana ya Ghana wenye umri wa chini ya umri wa miaka 17 maarufu kwa jina la Black Starlets, inatarajiwa kutua kesho Jumamosi Aprili mosi saa 9.40 usiku kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya wenyeji Serengeti Boys ambayo ni timu ya taifa ya vijana ya Tanzania.
 

Mchezo huo wa kirafiki wa kimataifa, kati ya wageni The Black Starlets na Serengeti Boys unatarajiwa kufanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam saa 10.00 jioni. Timu hiyo itafikia Hoteli ya Southern Sun jijini Dar es Salaam.


Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
 

http://tff.or.tz/news/839-ghana-kutua-serengeti-boys-kuivaa-tena-burundi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni