.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 30 Aprili 2017

BONDIA ANTHONY JOSHUA AMALIZA NGEBE ZA WLADIMIR KLITSCHKO KWA KO

Bondia Anthony Joshua amechezea vizuri pambano la jana usiku na kujiongezea mkanda wa uzito wa juu wa WBA huku akiwa na mkanda wa IBF, baada ya kumtoa KO bondia Wladimir Klitschko katika pambano lililofanyika kwenye dimba la Wembley.

Katika pambano hilo lililoshuhudiwa na mashabiki 90,000, bondia Joshua alimuangusha chini Klitschko katika raundi ya tano kabla ya yeye pia kuangushwa chini kwa mara ya kwanza kati ya mapambano yake 19 katika raundi ya sita ya mchezo huo.

Mabondia hao wate wawili walionekana kuwa ni hatari katika raoundi mbili za mwanzo ambazo hazitosahaulika katika kumbukumbu za ngumi, kabla ya Joshua kumsimamisha Klitschko katika raundi ya 11.
                                Bondia Anthony Joshua akimshindilia ngumi bondia Wladimir Klitschko
Bondia Wladimir Klitschko akiwa ameenda chini huku refa akimzuia Anthony Joshua asilete maafa zaidi
Bondia Anthony Joshua akiwa chini baada ya kupigwa ngumi nzito na bondia Wladimir Klitschko
Bondia Anthony Joshua akiwa amempa konde lililomuingia barabara bondi Wladimir Klitschko
Bondia Anthony Joshua akishangilia baada ya kumdunda bondi Wladimir Klitschko aliyechini

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni