.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 26 Aprili 2017

CHELSEA YAIFUNGA SOUTHMPTON NA KUJIKITA KILELENI MWA LIGI

Timu ya Chelsea imeendelea kujikita kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza kwa tofauti ya pointi saba baada ya kupata ushindi mzuri wa magoli 4-2 dhidi ya Southampton katika dimba la Stamford Bridge.

Katika mchezo huo Eden Hazard na Diego Costa walishuka katika kikosi cha kwanza na ilimchukua dakika tano tu Hazard kuifungia Chelsea goli la kwanza, lakini mchezaji wa zamani wa Chelsea Oriol Romeu alisawazisha goli hilo.

Gary Cahill aliifungia Chelsea goli la pili na kisha Diego Costa akaongeza goli la tatu katika dakika ya 53 na kufunga la nne dakika ya 89, kabla ya mchezaji mwingine wa zamani wa Chelsea Ryan Bertrand kuifungia Soumpton goli la pili katika dakika ya 90+4.
                          Eden Hazard akiifungia Chelsea goli la kwanza katika mchezo huo
                                Mshambuliaji nyota Diego Costa akifunga goli la tatu la Chelsea
   N'Golo Kante akimchezea rafu Ward-Prowse na kujikuta akiambulia kadi ya njano 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni