Wakazi wa Gongolamboto wakipita katika
daraja ambalo kingo zake zimesombwa na mafuriko barabara ya kuelekea
Machinjio ya Pugu Kajiungeni Dar es Salaam leo.
Mwonekano wa eneo hilo baada ya kingo
kusombwa na maji ya mafuriko
Daladala likipita kwenye daraja hilo
ambalo kingo zake zimesombwa na mafuriko
Na. Mtandao wa Habari za Jamii
MANISPAA ya Ilala imeombwa kufanya
jitihada za makusudi kuinusuru daraja linaloungani eneo la Gongola
mboto na Machinjio ya Pugu ambalo lipokatika hatari ya kusombwa na
maji.
Wito huo umetolewa Dar es Salaam leo na
wakazi wa Pugu Machinjioni ambao wamesema iwapo hatua za haraka
hazitachukuliwa mawasiliano kati ya wananchi wa eneo hilo na
Gongolamboto yatatoweka hivyo kuwa adha kwao kwa kufika makwao kwa
kupitia Pugu Kajiungeni badala ya barabara ya Gongo lamboto Pugu
Machinjioni kupitia kiwandacha kutengeneza nguo cha Namera.
Tunaomba manispaa yetu ilifanyie
ukarabati daraja hili ambapo kwa sehemu kubwa kingo zake zimesombwa
na maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha " alisema Omari
Mshamu mkazi wa eneo hilo.
Mkazi mwingine wa eneo hilo Marietha
Stanslaus alisema iwapo daraja hilo linasombwa na maji watakaopata
shida zaidi ni wanafunzi kwani watalazimika kutumia njia ndefu kufika
mashuleni kwao kutokana kuwa wengi wao wanasoma shule za
Gongolamboto.
Jithada za kumpata diwani wa eneo hilo
ili kuzungumzia suala hilo zilishindika baadaya kupiga simu yake
ambayo haikupatikana. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za
jamii.com-simu namba (0712-727062)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni