Mtoto wa kiume wa miaka miwili
aliyekuja kuwa maarufu kimataifa baada ya kuwa na tabia ya kuvuta
zigara katika kijiji kimoja nchini Indonesia ameacha tabia hiyo na
kupungua uzito na sasa amekuwa anafanya vizuri katika shule
anayosoma.
Mtoto huyo Aldi Rizal alipata
umaarufu mnano mwaka 2010 alipogundulika katika kijiji kimoja
masikini huko Sumatra, Indonesia, akivuta sigara 40 kwa siku huku
akiendesha kigari cha watoto.
Miaka miwili baadaye mtoto huyo
aliacha tabia hiyo ya uvutaji sigara kwa msaada wa serikali ya
Indonesian kwa kumpatia tiba maalum ya kuondokana na tabia hiyo, na
kufanikiwa kuachana kabisa na uvutaji sigara.
Mtoto Aldi Rizal akivuta sigara yake huku akiendesha kigari cha watoto
Mtoto Aldi Rizal anavyoonekana sasa akiwa na umri wa mika tisa
Mtoto Aldi Rizal akicheza shuleni hivi sasa amekuwa ni mwenye tabia nzuri




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni