Rais Uhuru Kenyatta amewaomba radhi
wa Kenya kutokana na chama cha Jubilee kujiandaa chini ya kiwango
wakati wa kura za mchujo jana na kusababisha kuhairishwa kwa zoezi
hilo katika kaunti zote 21.
Akiongea Ikulu, rais Uhuru amesema
hakutarajia kujitokeza kwa wapigakura wengi kiasi hicho,
waliosababisha kuibuka kwa upungufu wa karatasi za kupigia kura
kwenye vituo vya kupigia kura.
Amesema chama cha Jubilee
kitaendesha uchaguzi huru na wahaki na kuongeza kuwa yupo tayari
kufuata matakwa ya wapigakura katika chaguzi za mchujo wa wagombea wa
nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni