.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 23 Aprili 2017

UVUMI WA DAVID DE GEA KUTIMKIA HISPANIA WAZIDI KUSHIKA KASI

Kipa wa Manchester United David De Gea amechochea uvumi zaidi unaomuhusisha na kuhamia klabu ya Real Madrid baada ya kutangaza kuuza jumba lake lililopo katika Jiji la Manchester.

Kipa huyo Mhispania aliyejiunga na United akitokea Atletico Madrid mwaka 2011, amekuwa mara kwa mara akihusishwa na mpango wa kurejea nchini kwao, ambapo mwaka 2015 alishindwa kuhama kutokana na makosa ya kimkataba.

Uvumi wa uwezekano wa De Gea kurejea Hispania haujamalizika, hii ni baada ya gazeti la The Sun kuripoti kuwa kipa huyo ameliweka sokoni jumba lake lenye thamani ya paundi milioni 3.85.
       Jumba la David De Gea analodaiwa kuliuza lenye thamani ya paundi milioni 3.85


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni