Timu ya Cleveland Cavaliers imefufua
matumaini katika michezo ya fainali ya NBA baada ya kuinyima ushindi
Golden State Warriors baada ya kuibuka na ushindi waliokuwa
wakiuhitaji katika mchezo wa fainali ya nne.
Katika mchezo huo wa jana mabingwa
hao watetezi Cleveland waliibuka na ushindi wa pointi 137-116,
matokeo yanayoifanya Warriors kuongoza kwa ushindi wa 3-1 dhidi ya
Cavaliers.
Katika mchezo huo ulioshudiwa na
mastaa kibao Kyrie Irving alifunga pointi 40 huku LeBron James
akifunga pointi 31 na kumaliza ubabe wa Golden State Warriors wa
kuwafunga katika michezo mitatu ya awali ya fainali.
Hata hivyo Golden Sate Warriors
wanaweza kuutwa ubingwa wa NBA nyumbani watakapokutana tena katika
mchezo wa tano wa fainali siku ya jumanne.
Lebron James akiruka juu na kufunga kikapu katika mchezo huo
Kris Jenner, Khloe Kardashian na
Kourtney Kardashian wakifurahi ushindi wa Cleveland Cavalier
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni