Wanaume wanne Afrika Kusini
wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa na makosa ya kula nyama za watu,
baada ya mmoja wao kujipeleka mwenyewe katika kituo cha polisi na
kusema amechoka kula nyama za binadamu.
Polisi walipomhoji mtu huyo
aliwaonyesha mguu wa mtu na mkono wa mtu na ndipo walipoenda naye
kwenye nyumba yake iliyopo KwaZulu-Natal, ambapo miili zaidi ya watu
ilipatikana na kuwakamata wanaume hao wakiwemo waganga wawili wa
jadi.
Msemaji wa polisi ameviambia vyombo
vya habari imesema wanaume hao wanne wanaumri wa miaka kati ya miaka
22 na 32 ni sehemu ya genge kubwa la wala watu.
Uchunguzi bado unaendelea huku
Polisi wakiwahimiza watu ambao ndugu zao wamepotea wajitokeze.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni