.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 27 Oktoba 2017

MADAKTARI INDIA WAFANIKIWA KUTENGANISHA MAPACHA WALIOUNGANA VICHWA

Madaktari bingwa wa upasuaji nchini India katika Jiji la Delhi wamefanikiwa kuwatenganisha watoto mapacha walioungana vichwa.

Watoto hao wa mwaka mmoja waitwao Jaga na Kalia wamefanyiwa upasuaji kwa muda wa saa 16, na kwa sasa wapo kwenye chumba cha wagonjwa mahututi, kwa mujibu wa madaktari.

Timu ya madaktari 30 waliofanya upasuaji huo wote wanatoka Taasisi ya Sayansi ya Tiba ya nchini India.

Watoto hao mapacha wanaume walizaliwa wakiwa wamechangia mishipa ya damu na mishipa midogo ya kwenye ubongo.
         Mmoja wa watoto mapacha walioungana kichwani akiwa amelala baada ya kutenganishwa

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni