.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 22 Januari 2018

MAJALIWA AHITIMISHA ZIARA YA MKOA WA MARA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe kuzindua mabweni mawili ya Magufuli na Majaliwa katika Shule ya Sekondari ya Bumagi wilayani Butiama Januari 20, 2018. Watatu kulia ni mkewe Mary.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi baada ya kuzindua mabweni mawili yaliyopewa majina ya Magufuli na Majaliwa katika shule ya Secondari ya Bumagi wilayani Butiama Januari 20, 2018. Wapili kushoto ni mkewe Mary.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Butiama, Nimrod Mkono (katikati) na mkewe Marylouise Januari 202018,kabla ya kumkabidhi mbunge huyo cheti cha shukurani kilichotolewa na wilaya ya Butiama ili kuthami mchango wake mkubwa wa kujenga na kuchangia maendeleo ya elimu wilayani humo. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Chuo Kikuu cha Julius Kambarage Nyerere ambacho kilichojengwa na mbunge huyo kikiwa ni sekondari na kutokana na ubora wake kilibadilishwa kuwa Chuo Kikuu.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Mbuge wa Butiama, Nimrod Mkono cheti cha shukurani kilichotolewa na wilaya ya Butiama ili kuthami mchango wake mkubwa wa kujenga na kuchangia maendeleo ya elimu wilayani humo. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Chuo Kikuu cha Julius Kambarage Nyerere kilichojengwa na mbunge huyo kikiwa na sekonda na kutokana na ubora wake kilibadilishwa kuwa Chuo Kikuu.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mbunge wa Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhungo katika mkutano wa hadhara aliouhutubia kwenye kijiji cha Muragi Januari 21, 2018.
Wananchi wa Kijiji cha Muragi wilayani Musoma Vijijini wakimshangilia Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia mkutano wa hadhara katika kijiji hicho Januari 21, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi na viongozi wa mkoa wa Mara katika kikao cha majumuisho ya ziara yake ya siku saba mkoani humo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkoa wa Mara mjini Msoma Januari 21, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiaagana na viongozi wa mkoa wa Mara kwenye uwanja wa ndege wa Musoma baada ya kukamilisha ziara ya siku saba mkoani humo Januari 21, 2017. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza alikopitia akitoka Musoma kwenda Dar es salaam Januari 21, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni