.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 28 Februari 2018

USAIN BOLT KUSHUKA DIMBANI KUSAKATA SOKO OLD TRAFFORD

Mwanariadha Usain Bolt anatarajiwa kucheza katika kikosi cha wachezaji 11 wa dunia dhidi ya wachezaji 11 wa Uingereza watakaoongozwa na Robbie Williams katika mechi ya kuchangisha fedha itakayochezwa kwenye dimba la Old Trafford, Juni 10 mwaka huu.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa mwanariadha huyo aliyestaafu mbio kucheza soka katika dimba la klabu anayoipenda ya Manchester United, huku mshindi huyo wa medali nane za dhahabu katika Olimpiki akitarajiwa kuwa kivutio miongoni mwa nyota wa mchezo huo.

Orodha ya vikosi hivyo vya mchezo huo wa kuchangisha fedha ulioandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Watoto- UNICEF, vitahusisha nyota wa soka na mastaa wa tasnia za burudani utachezwa siku nne kabla ya kuanza michuano ya kombe la dunia Urusi.

Nyota huyo Mjamaica Bolt mwenye umri wa miaka 31, jana aliibua uvumi kwa watu wanaomfuatilia kwenye mitandao ya jamii baada ya kuandika kuwa ametia saini kuchezea klabu ya soka, na watu kuhisi kuwa amejiunga na Manchester United.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni