.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 15 Machi 2018

ANTONIO CONTE AHISI KIPIGO WALICHOPATA NI CHA UONEVU

Kocha wa Chelsea Antonio Conte anahisi kipigo cha magoli 3-0 kutoka kwa Barcelona kilichoitoa timu yake katika Ligi ya Mabingwa Ulaya hakikuwa cha “haki”.

Magoli mawili kutoka kwa Lionel Messi pamoja na mmoja kutoka kwa Ousmane Dembele likiwa goli lake la kwanza akiwa na Barcelona yalitosha kufanya matokeo ya jumla kuwa 4-1.

Kipigo hicho kimeathiri nafasi ya Chelsea kucheza michuano hiyo msimu ujao, ambapo sasa itabidi wapigane kumaliza ligi Kuu ya Uingereza katika nafasi nne za juu.
                          Lionel Messi akifunga goli lake la kanza ndani ya dakika tatu tu ya mchezo
Ousmane Dembele akifunga goli la pili la Barcelona likiwa ni goli lake la kwanza tangu ajiunge na timu hiyo
Kocha wa Chelsea Antonio Conte akimpongeza Lionel Messi kwa kumkumbatia baada ya kumalizika mechi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni