Mshambuliaji nyota Romelu Lukaku
amefunga goli lake la 12 katika michezo 11 ya Kombe la FA, wakati
Manchester United ikiifunga Brighton magoli 2-0 na kutinga nusu
fainali ya kombe hilo.
Lukaku alifunga goli la kwanza kwa
kichwa akiunganisha krosi ya Nemanja Matic, ambaye alifunga goli la
ushindi la dakika za mwisho kufuatia mpira wa adhabu uliopigwa na
Ashley Young.
Ushindi huo unaongeza matumaini ya
Manchester United kutwaa kombe hilo baada ya kutolewa Ligi ya
Mabingwa Ulaya jumanne na Sevilla, huku wakiendeleza rekodi ya
kutofungwa goli katika michuano ya FA msimu huu.
Mshambuliaji nyota wa Manchester United Romelu Lukaku akifunga goli la kwanza kwa mpira wa kichwa
Kiungo mkabaji Nemanja Matic akifunga goli la pili la Manchester United
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni