.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 20 Aprili 2018

WASIOLIPA KODI YA ARDHI KUCHUKULIWA HATUA

Na Mahmoud Ahmad,Arusha.

Kamishna Msaidizi wa Ardhi kanda ya Kaskazini Leo Komba amesema kuwa serikali itawachukulia hatua wamiliki wa ardhi wasiolipa kodi ya ardhi kwa mujibu wa sharia ya ardhi Namba 4 ya mwaka 1999 hivyo amewataka kulipa kodi hiyo kwa wakati ili kuepuka kufikishwa mahakamani.

Akizungumza jijini Arusha Komba alisema kuwa wizara imejipanga kikamilifu kusimamia taratibu za kuwafikisha mahakamani wadaiwa wote watakaokaidi kulipa kodi ya ardhi na kukusanya kodi ya pango la ardhi kwa kila kipande cha ardhi kilichomilikishwa kwa mujibu wa sharia.

Aidha alisema kuwa Wizara imerahisisha ulipaji wa kodi ya pango la ardhi ambapo mmiliki akishapata Ankara ya madai anaweza kulipa kwa kutumia simu ya kiganjani .

“Pamoja na suala zima la ulipaji kodi la Ardhi ,Mhe.Waziri wa Ardhi ameanzisha kampeni ya Funguka kwa Waziri wa ardhi kuondoa migogoro ya ardhi ,Hivyo wale wananchi wenye kero za ardhi wanatakiwa kujaza fomu ambazo zipo kwenye ofisi zote za Halmashauri na Ofisi za wakuu wa Wilaya ili Waziri atatue kero hizo” Alisema Kamishna

Naye Afisa Ardhi Mwandamizi Thadeus Riziki amesema kuwa ardhi ambazo hutozwa kodi hiyo ni zile ardhi ambazo zimepimwa na zina hatimiliki,maeneo ambayo hayajapimwa mengi hayajaingizwa katika mpango wa kulipa kodi.

Afisa huyo alisema kuwa serikali ina mpango wa kupima maeneo ambayo hayapimwa na pia kurasimisha makazi holela ili waweze kupatiwa huduma muhimu za kijamii.

Alisema kuwa ni vyema wananchi wakajijengea utaratibu wa kulipa kodi kwa wakati ili kuepuka usumbufu ikiwemo kufikishwa mahakamani .

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni