.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 8 Desemba 2013

RAIA WA AFRIKA KUSINI WAKUSANYIKA NYUMBA ZA IBADA KUMUOMBEA MANDELA


Wananchi wa Afrika Kusini wamekusanyika kwenye makanisa, misikiti pamoja na kwenye mahekalu ya ibada hii leo kumkumbuka na kumuombea aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela, ambaye ujumbe wake wa amani na mapatano ulijenga umoja katika taifa hilo.


Maombi hayo ya kitaifa yanafungua rasmi maombolezo ya wiki moja kabla ya maziko ya kitaifa ya kiongozi huyo aliyefanikiwa kuvunja ubaguzi wa makaburu nchini Afrika Kusini wakati wa zama za ubaguzi, na kujenga taifa lenye kuzingatia usawa na demokrasia.



Rais Barack Obama wa Marekani na mkewe Michelle watahudhuria ibada ya kumbukumbu ya Mandela siku ya Jumanne Jijini Johannesburg, huku idadi kubwa ya viongozi wa dunia wakitarajiwa kwenda Afrika Kusini kutoa heshima zao za mwisho kwa shujaa huyo wa vita vya ubaguzi.



                 Mke wa zamani wa Mandela, Winnie Madikizela-Mandela


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni