![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrfehJJFqvd0qT99kMPV7tRoC-Rp6OS85625o-Lz4BnoeAzRJJx5I7_9a8G6D2zsELG3dJxgj8pbFQ0KOMfBu5OcrhJ5Y6Y3aKgzSnOAmPelS6nXaQ4R1aoL7JkJ81cqGT3wFrM19YJJA/s640/jkuhuru.jpg)
Hayo yamesemwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati akizungumza
kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 52 ya uhuru yaliyofanyika kitaifa
hii leo katika uwanja wa uhuru jijini Dar esa Salaam
Rais Kikwete amesema marehemu mzee
Mandela alikuwa ni kiongozi wa pekee aliyepigania maslahi ya waafrika
hasa weusi bila kujali kuhatarisha uhai wake, na ikumbukwe kuwa wakati
anapigania kuondoa ubaguzi wa rangi, alikuwa akifanya katika mazingira
magumu kwa kuwa ukatili na utesaji wa waafrika weusi ulikuwa kwa kiwango
cha hali ya juu
"Lakini mzee Mandela alikuwa amekubali
kujitoa muhanga, alipambana na ukatili huo bila woga, kama ni kufa wacha
nife lakini sitaogopa kuwatetea waafrika, kwa kweli ndugu zangu
tumempoteza kiongozi shujaa wa kweli aliyepambana na makaburu bila woga"
alisema Kikwete
Amesema kitendo cha kiungwana
alichokifanya marehemu Mzee Mandela baada ya kutoka jela cha kuwasamehe
wale wote waliomtesa na hata kumfunga jela ni cha kipekee na kina funzo
kubwa kwa wananchi na viongozi wote duniani, akimaanisha hakuna haja ya
kulipisha kisasi
"Tupo watu hapa tuliopanga kulipiza
kisasi, nikipata watanikoma, kiukweli kisasi hakisaidii tujifunze
kupitia kwa Mzee Mandela, hakulipiza kisasi, na sisi tusilipize kisasi"
alisema Rais Kikwete
Ucheshi
na upendo aliokuwa nao Mzee Mandela kwa dunia, ni dhahiri kuwa viongzoi
wote wa mataifa makubwa na hata madogo yatafika Afrika Kusini kumzika
marehemu Mzee Mandela anayetarajiwa kuzikwa Jumapili Desema 15 mwaka huu
huko nchini Afrika kusini
Kwa hisani ua Masama Blog
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni