Mamlaka
ya Palestina imeendesha hafla ya sherehe za ndoa za kufungwa pamoja
kwa wanandoa 300 katika Ukanda wa Magharibi wa Gaza.
Rais
wa Palestina Mahmoud Abbas amehudhuria sherehe ya kufungisha ndoa za
pamoja kwa wanandoa 218 katika Mji wa Jericho. Ndoa zingine za
pamoja kwa wanandoa 80 zimefanyika eneo la Gaza.
Rais
Abbas amesema mamlaka ya Palestina imetumia kiasi cha dola milioni
1.5 kugharamia ndoa hizo ikiwemo zawadi ya dola 4,000 kwa kila
mwanandoa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni