Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu imewaachia huru Mhariri Mtendaji wa kampuni ya New
Habari, Absalom Kibanda, Meneja Uendelezaji Biashara wa Kampuni ya
Mwananchi Communication Limited Theophil Makunga na mwandishi Samson
Mwigamba.
Akisoma hukumu
hiyo Jijini Dar es Salaam, Hakimu Mkazi Warialwande Lema amesema
washtakiwa hao walishtakiwa kwa hisia tu na hisia haziwezi kuwa na
mashiko hata zikiwa na nguvu ya aina gani na kuongeza kuwa ushahidi
uliowasilishwa dhidi yao ulikuwa dhaifu.
Makunga na wenzake Absalom Kibanda na
Samson Mwigamba walikuwa wanakabiliwa na kesi ya uchochezi dhidi ya
askari wa majeshi ya ulinzi kwa kuchapisha makala kwenye gazeti la
Tanzania Daima yenye maneno yaliyolenga kuwashawishi wasitii viongozi
wao.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni