Polisi
katika kaunti ya Turkana nchini Kenya wamemuachia huru mwanamke mmoja
aliyechinja mbwa wawili na kula nyama zao na familia yake ili kuweza
kuishi kutokana na njaa kali iliyopo kwenye kaunti hiyo.
Mwanamke
huyo Akai Ekomua alisema kisa cha kuchinja mbwa wake ni ili apate
nyama ya kula na familia yake iliyopo kwenye njaa na pia aliwagaiwia
majirani zake nao ili wajinusuru na baa la njaa.
Mwanamke
huyo aliyefiwa na watoto watatu kutokana na njaa hiyo, amelieleza
jeshi la polisi kuwa aliamua kuchinja mbwa hao, kwa kuwa aliogopa
kuvunja sheria iwapo angeiba mbuzi kwa majirani zake.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni