.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 12 Machi 2014

SEPP BLATTER ASEMA HAKUNA KUTOA HOTUBA UFUNGUZI WA KOMBE LA DUNIA


Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limetangaza kuwa hakutakuwa na suala la kutolewa hotuba katika sherehe za ufunguzi wa Kombe la Dunia mwezi Juni mwaka huu.

Mwaka jana Rais wa Brazil Dilma Rousseff alizomewa na mashabiki wa mpira katika ufunguzi wa Kombe la Shirikisho, ambalo huanza kabla ya michuano ya Kombe la Dunia.

Katika mahojiano na Shirika la Habari la DPA, Rais wa Fifa Sepp Blatter ameonyesha kusikitishwa na hali ya kukosekana kwa utulivu nchini Brazil, hata hivyo anatarajia michuano ya Kombe la Dunia itatuliza hali hiyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni